WELCOME

"Experience is not what happens to you; it is what you do with what happens to you." and "When you feel like giving up, remember why you held on for so long in the first place"Instead of giving myself reasons why I can't, I give myself reasons why I can." because always "When one door closes another door opens; but we so often look so long and so regretfully upon the closed door, that we do not see the ones which open for us."by ISI H


Friday, January 25, 2013

BAADHI YA MATUKIO YA PICHA KATIKA MAADHIMISHO YA KUZALIWA MTUME MUHAMMAD S.W.A MKOANI ZANZIBAR


Ustadh Rashid Jaffer wa Magogoni Mjini Zanzibar,akisoma Quran Tukufu ya Ufunguzi wa Maulid ya Kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyosomwa jana katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar,ambapo kila mwaka hufanyika Maulid kama hayo na kuhudhuriwa na maelfu ya Wumini wa Dini ya Kiislamu.
Ustadh Abdulla Hamad wa Chuo cha Kiislamu,akitoa tafsiri ya Aya za Quran,zilizosomwa na Ustadh Rashid Jaffer wa Magogoni Mjini Zanzibar,akisoma Quran Tukufu ya Ufunguzi wa Maulid ya Kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyosomwa jana katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar,ambapo kila mwaka hufanyika Maulid kama hayo na kuhudhuriwa na maelfu ya Wumini wa Dini ya Kiislamu.
Mtafsiri Lugha kwa njia ya alama akitoa tafsiri ya maneno yanayozungumzwa wakati wa Hafla ya sherehe za Maulid ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.
Wake za Viongozi na Akinamama wakisikiliza Maulid Barzanj ya Kuzaliwa kwa yaliyosomwa na wasomaji mbali mbali na Qasida katika sherehe za Maulid ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu waliohudhuria katika sherehe za Maulid ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia) akitiwa Marashi wakati wa kumswalia Mtume (S.A.W) wakati wa sherehe ya Maulid ya Kuzaliwa kwake katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akifuatana na Viongozi wa Jumuiya ya Maulid EL Nabii Zanzibar,alipowasili katika viwanja vya Maisara katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhamad (S.A.W) yaliyofanyika jana.
Ustadh Ali Twalib Mohamed,wa Kibanda Hatari Mjini Zanzibar akisoma Maulid Barzanj Mlango wa kwanza katika kusherehekea kwa kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.

Friday, January 4, 2013

KWAHERI SAJUKI

Baada ya kuugua kwa muda mrefu, hatimaye aliyekuwa muigizaji wa filamu nchini, Juma Kilowoko maarufu kama Sajuki amefariki dunia jana alfajiri katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa Katibu wa chama cha waongoza Filamu Wilaya ya Ilala, Rajabu Amiri hivi karibuni Sajuki alikuwa anasumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu,mgongo na  kansa  ya ngozi

Sajuki alikuwa akitakiwa kurejea tena nchini India kwaajili ya kuendelea na matibabu ya tatizo lililokuwa likimsumbua ambapo jumla ya shilingi milioni 28 zilikuwa zikihitajika.

Hivi karibuni ilidaiwa kuwa alikuwa ameshakusanya shilingi milioni saba tu zilizotokana na michango ya watu na show alizokuwa akizifanya kukusanya fedha hizo. Show ya mwisho aliifanya jijini Arusha ambako alianguka kwenye stage.

Kifo hicho cha Sajuki kimepokelewa kwa masikitiko makubwa kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa Tanzania waliotumia mitandao ya kijamii kuelezea masikitiko yao.

Mwasiti Almas
Tunapolala na kuamka tunasema AHSANTE kwa mungu,tunapopoteza pia tunaowapenda tuseme AHSANTE… alichokileta ALLAH chini ya jua atakichukua

Salama A. Jabir
Mwenyezi Mungu Akusamehe Makosa Yako Ndugu Yetu Juma Kilowoko..Ucheshi Wako Ntaukumbuka Milele. Pumzika Kwa Amani Rafiki. #RIPSajuki

Jokate Mwegelo
Nimesikia hii habari sasa. Sad lakini kazi ya Mungu haina makosa tunazidi kumtumainia yeye na kumshukuru. Upumzike kwa amani sajuki. Amen!!

Zitto Zuberi Kabwe
Hali ya Afya ya Sajuki ndiyo ilinisukuma sana kuanza kusaidia wasanii nchini kupata kipato stahili na kazi Yao. Kifo chake kimeniondolea Mtu niliyemtazama kama kishawishi Cha Mimi kupigania haki za Watanzania walio kwenye entertainment industry. Sajuki left an indelible mark in my politics. Pumzika Kwa Amani Juma.

Masanja ‏Mkandamizaji

Duniani si nyumbani kwetu. Ni njia tu.

Hemedy Suleiman
R.I.P SAJUKI……..daaaaaah this is painful!!