WELCOME

"Experience is not what happens to you; it is what you do with what happens to you." and "When you feel like giving up, remember why you held on for so long in the first place"Instead of giving myself reasons why I can't, I give myself reasons why I can." because always "When one door closes another door opens; but we so often look so long and so regretfully upon the closed door, that we do not see the ones which open for us."by ISI H


Monday, August 19, 2013

HAYA ALIYASEMA LOWASA KUHUSU AJIRA TANZANIA

Lowasa ameyasema hayo jana jijini Mwanza wakati akizungumza na waumini wa Kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato kabla ya kuanzisha harambee maalum ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.
                                                               
Amesema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka 2006 unaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 12 ya vijana hawana ajira na wengi wa vijana hao wako mijini, asilimia 15 ya vijana nchini kati ya milioni 25 za vijana ndio wenye ajira, ilihali asilimia 70 ya vijana wenye umri kati ya miaka 13 -34 ni kundi kubwa ambalo ni tegemezi na halina ajira na hii ni kati ya nguvu kazi ya vijana milioni mbili na nusu ambao wako mijini na hawana ajira.
                                            
Amefafanua kuwa wakati hali hiyo ikitokea vijana 850,000 ambao wamekuwa wakihitimu elimu ya
msingi, sekondari na vyuo wakiwa tayari kuingia kwenye soko la ajira lakini inasikitisha kati ya hao, ni asilimi 5 tu ndio wanaopata ajira ya kudumu, huku asilimia 35 ikijikita katika kilimo ambacho bado kinakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo zile za uhaba wa pembejeo.

Amewataka watanzania wote kushirikiana na serikali kuhakikisha kuwa inawekwa mipango madhubuti kulinusuru kundi hilo kubwa la vijana wenye utayari wa kuingia kwenye ajira.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria harambee hiyo ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa zamani Nyamagana Lawrence Masha, Mbunge wa Rolya Lameck Airo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Christopher Mwita Gachuma, Mbunge wa zamani wa Jimbo la Busega(CCM) Dk. Raphael Chegeni na Mbunge wa sasa wa Nyamagana(Chadema) Ezekiah Dibogo Wenje.

                                                
Kwa upande wa uwakilishi wa Serikali uliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Said Amanzi na baadhi ya wafanyabiashara maarufu wa mikoa ya kanda ya ziwa na baadhi wazee maarufu.

Katika harambee hiyo ya kusisimua iliyoongozwa na Mbunge wa Monduli Mh.Edward Lowasa aliyetoa shilingi milioni 10 kama mchango wake, jumla ya shilingi milioni 200 zimepatikana hivyo kuvuka lengo la shilingi milioni 150, kumalizia Ujenzi wa Kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato Mwanza.

No comments:

Post a Comment