WELCOME

"Experience is not what happens to you; it is what you do with what happens to you." and "When you feel like giving up, remember why you held on for so long in the first place"Instead of giving myself reasons why I can't, I give myself reasons why I can." because always "When one door closes another door opens; but we so often look so long and so regretfully upon the closed door, that we do not see the ones which open for us."by ISI H


Friday, January 4, 2013

KWAHERI SAJUKI

Baada ya kuugua kwa muda mrefu, hatimaye aliyekuwa muigizaji wa filamu nchini, Juma Kilowoko maarufu kama Sajuki amefariki dunia jana alfajiri katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa Katibu wa chama cha waongoza Filamu Wilaya ya Ilala, Rajabu Amiri hivi karibuni Sajuki alikuwa anasumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu,mgongo na  kansa  ya ngozi

Sajuki alikuwa akitakiwa kurejea tena nchini India kwaajili ya kuendelea na matibabu ya tatizo lililokuwa likimsumbua ambapo jumla ya shilingi milioni 28 zilikuwa zikihitajika.

Hivi karibuni ilidaiwa kuwa alikuwa ameshakusanya shilingi milioni saba tu zilizotokana na michango ya watu na show alizokuwa akizifanya kukusanya fedha hizo. Show ya mwisho aliifanya jijini Arusha ambako alianguka kwenye stage.

Kifo hicho cha Sajuki kimepokelewa kwa masikitiko makubwa kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa Tanzania waliotumia mitandao ya kijamii kuelezea masikitiko yao.

Mwasiti Almas
Tunapolala na kuamka tunasema AHSANTE kwa mungu,tunapopoteza pia tunaowapenda tuseme AHSANTE… alichokileta ALLAH chini ya jua atakichukua

Salama A. Jabir
Mwenyezi Mungu Akusamehe Makosa Yako Ndugu Yetu Juma Kilowoko..Ucheshi Wako Ntaukumbuka Milele. Pumzika Kwa Amani Rafiki. #RIPSajuki

Jokate Mwegelo
Nimesikia hii habari sasa. Sad lakini kazi ya Mungu haina makosa tunazidi kumtumainia yeye na kumshukuru. Upumzike kwa amani sajuki. Amen!!

Zitto Zuberi Kabwe
Hali ya Afya ya Sajuki ndiyo ilinisukuma sana kuanza kusaidia wasanii nchini kupata kipato stahili na kazi Yao. Kifo chake kimeniondolea Mtu niliyemtazama kama kishawishi Cha Mimi kupigania haki za Watanzania walio kwenye entertainment industry. Sajuki left an indelible mark in my politics. Pumzika Kwa Amani Juma.

Masanja ‏Mkandamizaji

Duniani si nyumbani kwetu. Ni njia tu.

Hemedy Suleiman
R.I.P SAJUKI……..daaaaaah this is painful!!

No comments:

Post a Comment